Monday, November 2, 2015

MSIMAMO MEDIA .COM: MSIMAMO MEDIA .COM: True value Media: SIMULIZI YA ...

MSIMAMO MEDIA .COM: MSIMAMO MEDIA .COM: True value Media: SIMULIZI YA ...:   True value Media: SIMULIZI ya



SIMU YA
MAMA…Sehemu ya2
Na Ismail Mang’ola

“NITARUDI MAMA YANGU” Yalikuwa ni maelezo mafupi ya kijana
Advocate Suma Mtata aliyoyaona huenda yangemfariji mama yake ili atakapokuwa
ameondoka asije akawa na kinyongo na mwisho wa siku mambo yakamwendea kombo.
Safari ya Advocate Suma Mtata imeanza, lakini haijulikani ni
wapi Advocate amedhamiria kwenda, kingine ni kwamba ameamua kuondoka bila hata
ya kuwaaga baadhi ya ndugu zake wa karibu hata marafiki zake waliotokea
kupendana sana.
Muda na masaa alioupoteza kijijini hapo aliona kama ilikuwa
ni mikosi kwake, licha ya kwamba kazi ya kilimo ilikuwa ikimpatia kipato na
hata wakati Vijana wengi walipokuwa wakihaha kwa kusaka pesa za kuwasaidia
kipindi cha kiangazi, yeye aliishi kama miongoni mwa watoto waliokuwa na maisha
ya kweli.
Sasa anaamua kuyaacha maisha hayo ya kilimo na kwenda kutafuta
maisha aliyoyaona yatakuwa na kipato kikubwa tofauti na hayo aliyokuwa
akiyategemea, hivyo aliamini huko anakoenda maisha yangekuwa mazuri zaidi ya
haya, akaondoka. Sasa endelea… *** Aliamini kwamba safari yake hiyo isingekuwa
ya maeneo ya karibu na mkoa wake alikotokea, dhamira ilikuwa ni kwenda kuishi
katika miji mikubwa moja ya miji hiyo ambayo aliiweka akilini mwake ni pamoja
na jiji la Dar es Salaam, Arusha na Jiji la Mwanza, maarufu ‘Rocky City.
Mbali na miji hiyo, pia aliutambua mji uliokuwa unaendelea
kukua kibiashara na kiuchumi mji wa Mbeya, huko Advocate Suma Mtata napo aliona
iwapo kama ataweza kuyazoea mazingira ya hali ya hewa, vilevile mawazo hayo
aliyaweka bayana kwenye akili yake.
Lakini hadi anaondoka kijijini hapo alikuwa bado hajapata
muafaka ni wapi anakokwenda na mji gani ambao ungeweza kumsaidia kuishi na
kufanya kazi ambayo itamuwezesha kupata kipato kikubwa zaidi ya kile alichokuwa
akikipata wakati akisahanya na kilimo.
Niukweli usiopingika kuwa, Advocate Suma Mtata alikuwa anapata
kipato kizuri katika harakati zake za kilimo. Labda alihitaji kubadilisha hali
ya upepo wa kipato hicho, kama tunavyojua, siku zote mwanadamu huwa haridhiki
na kile anachokipata, kwa kawaida ama kwa namna ninavyojua, unaweza kumpa
mshahara wa kutosha, lakini iwapo kama atasikia kuna sehemu wafanyakazi
wanalipwa juu ya ule anaolipwa kazini kwake, yuko tayari kwenda kufanyakazi
kwenye hiyo kampuni ambayo amesikia inalipa vizuri.
Hii ni kawaida kwa watanzania kufanya hivyo tena bila
kufikiria athari yake ni nini. Lakini ili mradi aachane na kipato hicho kidogo,
ndizo fikira za wengi wetu hapa nyumbani.
Majara ya saa nne Ikola anaenda nyumbani kwa kina Advocate
Suma Mtata, walikuwa na mipango yao ambayo walipanga jana yake kwa ajili ya
katika kijiji cha Ngamo kwa mjomba wake aambaye aliwaahidi angeenda
kuwatembelea baada ya kukutana mnadani.
“Mjomba usiwe na wasiwasi, nitakuja kuwatembeeni, hapa
katikati kuna vitu vilikuwa vimenibana sana mjomba, hivyo kwa sasa nahisi mambo
yameachia, kubwa naomba wasalimie nyumbani na uwahakikishie wiki hii nitakuja
kuwaona, najua ndugu zangu wamenikumbuka sana” Advocate Suma Mtata alimweleza
mjomba wake Mzee Hango kasha wakapeana mikono kwa minajili ya kuagana na
kuachana.
Ikola na Advocate Suma Mtata ni ndugu kwa upande wa mama zao,
mama yake na Advocate Suma ni mkubwa na mama yake na Ikola ni mdogo, wote
wamezaliwa tumbo moja na mzee Moghu.
Kwa hiyo walitambuana kuwa wote ni ndugu tena udugu wa ndani
kabisa. Lakini cha kushangaza, Ikola hakujua kama ndugu yake huyo, Advocate
Suma Mtata kama alikuwa na safari iliyokuwa imejificha, naamanisha hakumwambia
kama alikuwa anahitaji kusafiri siku za karibuni.
Pamoja na mipango hiyo ya kwenda Ngamu kwa mjomba Hango, bado
hakumweleza kama safari hiyo ilikuwa imeshaota mbawa, akamficha na mambo yake
yalipokuwa yamekamilika akalazimika kumuaga mama yake na dada yake Mwana pekee,
sio mabinamu zake wala wajomba wengine waliokuwa jirani na nyumbani kwao.
Majira ya saa kumi na mbili na robo, basi lililokuwa na namba
za usajili TZ 19171 lilifika katika stendi ya mabasi ya Kijota kisha akajitoma
ndani tayari kwa safari ya kuelekea katika mji mdogo wa Singida ambapo mwanzo
wa safari ya kuelekea miji mikubwa ndiko ilikokuwa inaanzia.
Basi alililopanda Advocate Suma Mtata ni basi ambalo lilikuwa
na sifa kubwa na kupelekea wanakijiji kulitungia nyimbo ambayo ilishika sana
hasa kwa wazee na Vijana waliokuwa wakinywa pombe za kienyeji.
Nakumbuka baada ya basi hilo kuwasili kwa mara ya kwanza
kijijini hapo, mbele liliandikwa ‘Singisa’ ambalo lilikuwa aina ya Layland,
lilikuwa na mlio mzuri sana, Vijana wengi waliupenda mlio wake na hata wakati
mwingine watu wengi waliweza kulitambua pale lilipokaribia kufika kijijini
likitokea mjini.
Lilikuwa na mngurumo wenye kusikika hata kama utakuwa mbali
kiasi gani, wengi waliweza kulitambua kuwa (Singisa inaingia) na kila lilipotua
kijijini hapo, Vijana kwa wazee na wale wa makamo waliweza kulishangilia na
kurukaruka utafikiri watoto wadogo, hali iliyoonyesha basi hilo lilipendwa
kupita maelezo ya kampuni iliyolitengeneza.
Kutoka kijijini hapo hadi mji mdogo wa Singida hapakuwa mbali
sana, ilikuwa ni umbali wa Maili moja, muda aliopanda basi hisi hilo kutoka
hapo hadi kufika mjini, lilitumia dakika sitini na tano kutokana na ubovu wa
miundombinu kipindi hicho ambapo barabara haikuwa nzuri, ilikuwa ni ya vumbi.
Hivyo mwendo wake usingeweza kuulinganisha na mwendo wa gari
linapokuwa kwenye barabara ya lami, ilikuwa ni shida sana kwa dereva kwenda
mwendo wa haraka, kwanza aliogopa kukata Springi, istoshe makorogesheni ya
ubovu huo wa barabara ilikuwa ni hatari kwa basi kuanguka hivyo ilibidi liende
mwendo wa kawaida.
Ikola alipofika nyumbani kwa mama yake mkubwa, alipoingia tu
ndani ya boma, aliuona mlango wa nyumba ya Advocate Suma Mtata ulikuwa
umefungwa na kufuli, akahisi labda atakuwa ameenda shambani kukata miwa, maana
wakati mwingine Advocate Suma Mtata alikuwa anapenda kwenda kushinda katika
shamba lao la miwa ambalo halikuwa mbali sana na hapo.
“Oooh mwanangu!!! Karibu baba” Mama yake na Advocate Suma
Mtata alimkaribisha Ikola mtoto wa mdogo wake, ‘Nyamaria’.
“Ahsante mama mkubwa, shikamoo mama” Ikola alimuamkia mama
yake mkubwa.
“Marhaaba mwanangu, Ikola! Habari za nyumbani” Mama
alimsalimia.
“Wote nyumbani hatujambo,mama sijui nyinyi huku”. Ikola
aliitikia na kisha naye akamrudishi salamu.
“Mwanangu huku hatujambo, ila kaka yako kaondoka!”
“Nani kaondoka?” Ikola alimuuliza mama yake mkubwa.
“Kaka yako Advocate Suma Mtata” akamjibu.
“Kaenda wapi?” Ikola akamuuliza tena.
“Mwanangu wee, hata haijulikani ni wapi ameenda, maana mimi
kaniambia kuwa amechoka kukaa hapa kijijini, hivyo ameona akatafute maisha huko
mijini, mwenyewe sijui kaenda mji gani ambako ameona atapata maisha mazuri”
Mama alimwelezea Ikola kwa kirefu kidogo.
“Inamaana hajakuambia ni wapi anaenda! Unataka kusema mama,
kajiondokea tu?” Ikola alimuuliza mama yake mkubwa kutaka kujua kwa undani zaidi.
“Kweli mwanangu, sijui hata moja zaidi ya pale aliponiambia
kuwa anataka kusafiri, na Habari ya safari yake kanieleza juzi jioni kashinda
jana na leo asubuhi nimeshangaa kuona mtu anagonga mlango wangu nilipoamka
nikamkuta ameshabeba bigi lake la nguo tayari kwa safari”. Mama aliendelea
kumweleza Ikola.
Mara kidogo akaingi Juma Shabani Nkumbi, Juma ni mtoto wa
kaka yake na Mama Advocate Suma Mtata wengi walipenda kumuita jina la mtoto
wake wa kwanza, anayeitwa ‘Mnyawi’ hivyo Bi. Mkubwa huyo akawa anaitwa kwa jina
hilo la mwanae wa kwanza ‘Nyamunyawi’ “Hodi” Juma alibisha hodi nyumbani kwa
shangazi yake”, baada ya kuingia ndani ya boma.
“Karibu mwanangu” Shangazi yake alimkaribisha.
“Shikamooo shangazi”. Juma alimuamkia shangazi yake Mama
Nyamunyawi.
“Mmeamkaje huku?” Juma alimsalimia shangazi yake.
“Sisi hatujambo mwanangu, nanyi hamjambo nyumbani?” Shangazi
yake naye akamrudishia salamu hiyo.
“Shangazi wote hawajambo” Juma naye akaipokea ile salamu na
kumjibu.
Baada ya salamu zile Juma aliamuulizia binamu yake Advocate
Suma Mtata kama alikuwepo wakati huo, alimiani kuwa alikuwa ndani kwa sababu
ilikuwa bado ni mapema hali ambayo asingekuwa na sehemu yeyote aliyeenda, kwani
kawaida vijijini iwapo kama mtu atakuwa ameenda mahali Fulani lazima wengi wao
watambue.
Hesabu ya wanavijiji hua inajulikana, kwanza ni uchache wa
wakazi pamoja na kutambuana kutokana na kila mkazi huonyesha upendo na
mshikamano wa kweli katika maisha yao hali ambayo inatofautiana na maisha ya
mijini.
“Mwanangu wee, mdogo wako hayupo! Kaondoka kwenda kutafuta
maisha huko alikoona atayapata”, Shangazi yake alimjibu.
“He! Kwani kaenda wapi?” Juma aliendelea kumuuliza shangazi
yake.
“Mwanangu hata najua basi, mwenyewe kasema atakapofika huko
safari yake itakapoishia ndipo atanijulisha kwa barua, lakini hadi anavuka
kizingiti hiki cha mlango hakuweza kuniambia ni wapi kaenda” Bi. Mkubwa huyo
alimweleza Juma mtoto wa kaka yake Mzee Shabani Nkumbi.
“Mhhhhh!” Juma alivuta pumzi na kimya cha sekunde kumi
kikafuata.
“Kwahiyo shangazi unataka kuniambia hajasema ni wapi anaenda!
Au kaenda Arusha? Maana siku nyingi alikuwa haachi kuahadithia mji wa Arusha”,
Juma aliendelea kumdadisi shangazi yake.
“Yaani mwanangu kukuambia ni wapi kaenda nitakuwa nmwenyewe
kasema akifika atakapoona hapo ndipo panamfaa ndipo atakapoandika barua na
kutujulisha ni wapi alipo lakini hadi anaondoka hapa, aliniacha nimeshika tama,
na hadi sasa namuwaza mwanangu, naona kama kaniacha mkiwa” Bi. Mkubwa
alioendelea kumjibu Juma.
“Shangazi acha mimi nirudi, maana kuna kazi nilitaka niifanye
pale nyumbani ya kufyetua matofali hivyo nilitaka nikasaidiane naye binamu
yangu, sasa kama hayupo ngoja nimfuate Munkulu kama nitamkuta?!” Juma alimjibu
shangazi na kisha akaaga na kuondoka.
Hali ile iliamsha upya mawazo kwa Bi. Mkubwa huyo namna ndugu
zake walivyokuwa hawakauki nyumbani hapo wakati Advocate Suma Mtata akiwepo,
Vijana wengi walipenda kumshirikisha katika kazi zao za kawaida kijijini hapo.


Hivyo Bi. Mkubwa alipomuona mtoto wa kaka yake kwenda
kumuulizia mwanae alihisi kama huko alikoenda ndio ulikuwa mwisho wa maisha
yake, lakini hakuwa na namna, Suma kashaondoka, kilichobaki ni kusubiri atarudi
ama ndio mwisho wake wa kuonana na ndugu zake hao.

No comments:

Post a Comment